Proverbs 4:1-6

Hekima Ni Bora Kupita Vitu Vyote


1 aSikilizeni wanangu, mafundisho ya baba yenu;
sikilizeni kwa makini na mpate ufahamu.

2 Ninawapa mafundisho ya maana,
kwa hiyo msiyaache mafundisho yangu.

3 bNilipokuwa mvulana mdogo katika nyumba ya baba yangu,
ningali mchanga na mtoto pekee kwa mama yangu,

4 cbaba alinifundisha akisema,
“Yashike maneno yangu yote kwa moyo wako wote;
yashike maagizo yangu na wewe utaishi.

5 dPata hekima, pata ufahamu;
usiyasahau maneno yangu wala usiyaache.

6 eUsimwache hekima naye atakuweka salama;
mpende, naye atakulinda.
Copyright information for SwhKC